Menu

Mario Balotelli
Mchezaji mtukutu kutoka AC Milan anatarajiwa kujiunga na timu ya Liverpool muda wowote baada ya ada ya uhamisho Pauni 16 milioni kukubaliwa. 
Hata hivyo swala ambalo analiogopa kocha wa Liverpool  Brendan Rodgers ni mwenendo wa tabia ya mchezaji huyo anapokuwa nje au ndani ya uwanja. 
Balotelli amekuwa mchezaji mwenye vituko sana na jazba, na hapendi kuonewa.
 Vikwazo vilivyokuwepo kwa sasa ni makubaliano ya
 kimkataba ambayo yatamuhusu yeye Balotelli na myenendo yake kitabia. Hilo likifikwa muafaka basi dakika yoyote, atatua Anfield. Kinachotia matumaini ni mchezaji huyo tayari amewaaga wachezaji wenzake kwamba anaiacha club yao muda wowote kuanzia sasa, na ameshawaaga hata wafanyakazi wengine.

0 comments:

Post a Comment

 
Top