Menu

Hivi Manchester united wanatumia mbinu za kisiasa kucheza mpira?
Nilikuwa najiuliza hilo swali lakini baadae nikapata majibu yakutosha.


 Najua unafahamu Manchester United chimbuko lake wapi! Ni Uingereza, hivi huwa unaona jinsi uingereza (England) ikiwa inajiandaa kama vile kombe la Dunia? Kuna timu itakayoonyesha mbwembwe kama uingereza kabla hata mashindano hayajaanza? Magazeti yataandika habari hata ambazo zikisema Rooney alikuwa anakula apple kabla ya mazoezi, au mchezaji Fulani maarufu eti kaenda kununua perfume Fulani supermarket kabla ya mechi!, habari ambazo hata uwanjani hazitahitajika. Basi tu ndo walivyo na mbwembwe zao kuonekana wenyewe ndo wanajua starehe kuliko wengine ulimwenguni. Unakumbuka ile habari yao iliyosema wachezaji wao wameruhusiwa kwenda na wake zao? sisi inatuhusu nini? wachache wameoa pale, ila walimaanisha waende na wachumba zao wakale bata. Mbwembwe nje ya uwanja nyingi kuliko uwanjani. na hatimaye hutolewa mapemaa na kubaki kula bata kama ambavyo wamezoea, Nijibu tu umewahi kusikia udaku wowote kwa timu ngangari kama Ujerumani? Wanaoona kazi hata kuongea na waandishi wa habari, pia huonyesha furaha kwa hisia pale wanapofanikiwa baada ya ushindi!
Kuna swali jepesi tu jamaa mmoja ameuliza Man united ni mashetani walio potea au ni masimba dume walio lala?
wameanza msimu huu kwa mbwembwe huku wakishinda mechi za kjipima kama dume la simba, lakini kwenye ligue kilaiini wanafungika. walisema timu ipo imara sana, sasa hivi nasikia wanasema timu itachukua hata miezi 3 kuwa fiti, si unakumbuka yale ya Moyes?

Mbona timu yenye pesa zakutosha na wachezaji maradufu kama Manchester City hatuwasikiki kwenye vyombo vya habari na udaku kama Man United utafikiri hawana walezi. Utafananisha kiwango cha mmoja mmoja na wachezaji wa Man City? Majibu ni City watashinda kabla hata yakuingia uwanjani.

Ohh! Wananifanya nianze kuifananisha na timu ya Yanga nchini Tanzania ambayo inashangilia mapema na kuwapa kipaumbele wachezaji wa nje ambao hata hawajawahi kuwaona wakicheza uwanjani, chaajabu ndio wanao pewa sifa na huduma nzuri kulioko hata wengine muhimu ambao wengi wao ni wazawa.

0 comments:

Post a Comment

 
Top